Posted in Hadithi

MFALME IZANA- SEHEMU YA 1

JINA LA MTUNZI: Shung Thong Xhi Mawasiliano: 0623410370, 0693548469 INSTAGRAM: @Shungthong UTANGULIZI “IZANA” ni stori yenye visa vya kusisimua! Ikielezea mausiano na taratibu za jamii za kiafrika  ikihusisha migogoro ya kusisimua,visa vya mahusiano ya kimapenzi pamoja na nguvu za ajabu!.Ikiwa inaongelea jamii ya kiutawala wa kifalme iliyokuwa inaitwa mizi,ambayo ilikuwa kaskazini huko.Ilikuwa ni kipindi ambacho Wajerumani walikuwa wanajaribu kutanua utawala wao na kusababisha vita ambayo inapelekea jamii ya mizi kupoteza kiongozi wao waliyekuwa wana muita “Miziya” wakiwa na maana ya mtukufu mfalme! Jambo hilo linawashitua wengi! Na kuwaacha na maswali mengi yasiyo na majibu ya haraka ama majibu ya kufaa…

Soma zaidi..
Posted in Hadithi

Mawimbi

Patrick J. Massawe 0715 676249 Utangulizi. Fred Samson kijana mtanashati anakutana ndani ya basi la daladala na mwanadada mrembo, Mariana, wakati huo mvua kubwa inayesha upande wa nje. Lakini wanapofika mwisho wa safari yao, Mariana anamsitiri kumfunika kwa mwavuli wake ili asilowane. Hatimaye wanaongozana wote huku wakitambulishana, na safari yao inaishia kujenga uhusiano mzito wa kimapenzi ambao baadaye unaleta misukosuko mingi na karaha na kuhatarisha penzi lao! Endelea na hadithi hii ya kusisimua mpaka mwisho wake…. MVUA za masika zilikuwa zinaendelea kunyesha mfululizo ndani ya jiji la Dar es Salaam, na kulifanya liwe katika utulivu wa hali ya juu.  Ni…

Soma zaidi..
Posted in Hadithi

Mfalme wa Kinanda -2

KWA WASOMAJI WAPYA UTANGULIZI… Simulizi ya “Mfalme wa kinanda” ni simulizi ya kihistoria ambayo inaelezea namna mfumo wa siasa ya vyama vingi ulivyoingia kwenye nchi za kiafrika na kuratibiwa huku ukiua uzalendo wa viongozi wa kiafrika na kuzorotesha uchumi na afya za wananchi. Riwaya hii inaeleza kuwa kabla ya mfumo wa uchaguzi wa viongozi wanasiasa kuingizwa Afrika, nchi za kiafrika zilikuwa na mfumo wake wa kiutawala. Nchi za magharibi zikaanza kuwarubuni wanasiasa wa kiafrika ili waige mfumo wao wa siasa na kuwaahidi kuwapa fedha za msaada kwa ajili ya kufanyia uchaguzi na kutatulia shida zingine. Ndipo na wanasiasa wa nchi…

Soma zaidi..
Posted in Hadithi

Mfalme wa Kinanda-1

Mwandishi Grey Solver UTANGULIZI… Simulizi ya “Mfalme wa kinanda” ni simulizi ya kihistoria ambayo inaelezea namna mfumo wa siasa ya vyama vingi ulivyoingia kwenye nchi za kiafrika na kuratibiwa huku ukiua uzalendo wa viongozi wa kiafrika na kuzorotesha uchumi na afya za wananchi. Riwaya hii inaeleza kuwa kabla ya mfumo wa uchaguzi wa viongozi wanasiasa kuingizwa Afrika, nchi za kiafrika zilikuwa na mfumo wake wa kiutawala. Nchi za magharibi zikaanza kuwarubuni wanasiasa wa kiafrika ili waige mfumo wao wa siasa na kuwaahidi kuwapa fedha za msaada kwa ajili ya kufanyia uchaguzi na kutatulia shida zingine. Ndipo na wanasiasa wa nchi…

Soma zaidi..
Posted in Hadithi

CHANZO NI WEWE

Mwandishi, Ismaily Himu Chanzo ni wewe ni tamthiliya inayozungumzia athari za watoto wa mitaani na changamoto zinazowakumba hasa katika nchi zinazoendelea. Mtunzi ameonesha jinsi jamii nzima inavyohusika kwa namna moja au nyingine kuongezeka kwa watoto hawa pamoja na namna ya kutatua tatizo hili, lengo likiwa ni kuifanya jamii nzima iwajibike katika hili. Tatizo la watoto wa mitaaani limekuwa ni tatizo la kidunia, limekuwa ni tatizo kubwa hasa katika nchi zinazoendelea hasa za bara la Afrika na Asia ambako jamii kubwa ni masikini. Tatizo hili haliwezi kutatuliwa na mtu mmoja mmoja au kikundi fulani cha watu bali kwa jamii nzima kujumuika…

Soma zaidi..
Posted in Hadithi

Ushetani wa Alphonce

MTUNZI NA MWANDISHI Egidius Jack Matungwa   Ndege ya papa, ilizunguka mara tatu, juu ya anga la uwanja wa ndege, wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Dar. Hiyo ilikuwa ni ishala ya salamu kwa maelfu ya watu waliojumuika uwanjani hapo, wakimgoja mgeni adhimu, kiongozi wa juu kabisa ulimwenguni, wa dini ya Romani Katoliki, baba mtakatifu papa Carol Peter wa 16.      Ulinzi uliimalishwa. Maofisa wa vyombo vya ulinzi, na wananjeshi wa ngazi tofauti, walisambazwa kila kona ya uwanja, ili kuhakikisha hali ya usalama ni ya kulidhisha.     Viongozi mbalimbali wa dini na serikali, walijumuika kumpokea papa. Watu ambao hawakuweza kufika…

Soma zaidi..