Posted in Makala

Kongole Kikeke kueneza Kiswahili kwa miaka 20 BBC

Gadi Solomon, Swahili Hub Jicho la Kiswahili leo limetua kwa mtangazaji mahiri wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ambaye amejizolea umaarufu kwa namna anavyotumia sanaa kwenye utangazaji kwa kutumia lugha ya Kiswahili. Mtangazaji huyo kinara kama anavyojiita, amejizolea sifa kutoka nchi mbalimbali ambazo zinazungumza lugha ya Kiswahili Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zinazozungumza Kiswahili. Lugha ni Sanaa. Jicho la Kiswahili limeona jitihada binafsi za mtangazaji huyo ambaye ni Mtanzania, ametangaza Ijumaa mwishoni mwa wiki iliyopita kuacha kazi BBC na kwenda kuangalia fursa kwingine bila kutaja anahamia wapi. Kinara huyo wa utangazaji pia amewahi kufanya kazi hapa nchini kwenye…

Soma zaidi..
Posted in Makala

Mnara wa Babeli, chanzo cha lugha nyingi duniani

By Dk Levy Ikapita miaka mingi. Wana wa Nuhu nao wakazaa watoto wengi sana. Watoto wao walikua na kuzaa watoto wengi zaidi. Na hapo ndipo kukawa na watu wengi zaidi duniani. Mmoja wa watu hao alikuwa kijukuu wa Nuhu jina lake Nimrodi. Alikuwa mbaya aliyewinda na kuua wanyama na wanadamu. Nimrodi pia alijifanya mfalme atawale watu wengine. Mungu hakumpenda Nimrodi.Wakati huo watu wote waliongea lugha moja. Nimrodi alitaka awakusanye ili awatawale. Unajua alichofanya? Aliwaambia watu wajenge mji na ndani yake kuwepo na mnara mkubwa na mrefu sana.Hawa ndezi wa kale waliamini wakijenga mnara mrefu watafika mbinguni kwa Mungu. Bange za namna…

Soma zaidi..
Posted in Makala

Utunzaji wa fasihi kidigitali ni amali kwa kizazi kijacho

FASIHI ni njia moja ya kuendeleza utamaduni wa jamii ambao pia ni ujumla wa maisha ya jamii hiyo. Kupitia kwa fasihi, jamii huweza kuhifadhi na kuendeleza mila, desturi, miiko, itikadi au hata falsafa yake. Fasihi hutumiwa kutoa mafunzo mema, maarifa na hekima miongoni mwa wanajamii. Fasihi ambayo pia hufunzwa shuleni, inaweza kutumiwa kujenga hulka nzuri miongoni mwa wanafunzi. Kenya ni nchi iliyobarikiwa kuwa na jamii nyingi, na kwa hivyo kuna dafina kubwa ya fasihi iliyosheheni katika jamii hizo. Je, fasihi hii hutumiwa kikamilifu kuwaelekeza, kuwafunza, kuwakosoa au kuwaelimisha watoto wetu kama ilivyokuwa zamani? Jibu ni la, hasha. Sababu za sisi…

Soma zaidi..
Posted in Makala

Historia ya mtunzi mashuhuri Euphrase Kezilahabi

Euphrase Kezilahabi amezaliwa mkoa wa Mwanza. Amezaliwa 13 Aprili 1944 katika kijiji cha Namagondo kisiwani Ukerewe. Euphrase Kezilahabi ni mwandishi kutoka nchini Tanzania. Euphrase kezilahabi Lugha yake ya kwanza ni Kikerewe lakini huandika hasa kwa Kiswahili ambacho amekipanua kwa kutumia mitindo ya lugha yake ya asili. Baba yake anafahamika kwa jina la Vincent Tilibuzya. Baba yake Euphrase Kezilahabi alikuwa msimamizi wa kijiji. Euphrase Kezilahabi alikuwa na ndugu 10 yaani wavulana 5 na wasichana 5. Alisoma katika shule ya msingi Nakasayenge. Tangu 1957 alisoma Seminari ya kikatoliki ya Nyegezi aliyomaliza mwaka 1966. Mwaka1967 alijiandikisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akasoma…

Soma zaidi..
Posted in Makala

Historia ya Dkt. Muhammed Seif Khatib

Umbuji ni kijiji kilichopo pembezoni mwa Wilaya ya Kati, Muhammed Seif Khatib walizaliwa  tarehe 10 Mei, 1952, majira ya vuli. Kiuzawa, ubabani anatoka kwenye ukoo wenye asili ya kusini ya Makunduchi na Jambiani. Ndoa ya baba mzazi Seif Khatib na mama mzazi Tatu Kombo ilibarikiwa watoto wanne, wanawake wawili na wanaume wawili; Sijamini, Ali, Muhammed (marehemu) na kitindamimba Maimuna (marehemu). Bwana Seif alioa mke mwengine na kubarikiwa mtoto mwanamke aitwaye Rukia (marehemu). Mwandishi huyu ingawa alizaliwa kijijini lakini makuzi yake yalifinyangwa mjini. Alipata elimu yake ya Madrasa katika chuo cha bibi Mwanzena na baadaye kidogo Msikiti Barza. Elimu ya msingi…

Soma zaidi..
Posted in Makala

Historia ya mtunzi wa ushairi Haji Gora Haji

Haji Gora alizaliwa mwaka 1933 katika Kisiwa cha kale cha kihistoria cha Tumbatu kilichopo Kaskazini ya Unguja. Mwana kindakindaki huyu wa Tumbatu anatoka katika ukoo wa hali duni ya kimaisha watoto sita kwa upande wa mama mmoja na baba mmoja. Anao ndugu wanne wa mama mmoja na baba mbalimbali. Amepata elimu ya madrasa mjini Unguja kwa bibi Mwanadarini katika mtaa wa Vuga. Alimaliza elimu ya Qur’an katika madrasa ya Maalim Ibrahim Juma Ngwali Kisiwani Tumbatu. Mazingira ya kisiwa cha Tumbatu ni ya shughuli za uvuvi na utwesi wa majahazi ya kusafiria. Mapema ya alfajiri ya maisha yake katika umri wa…

Soma zaidi..