Category: Makala
Historia ya Dkt. Muhammed Seif Khatib
Umbuji ni kijiji kilichopo pembezoni mwa Wilaya ya Kati, Muhammed Seif Khatib walizaliwa tarehe 10 Mei, 1952, majira ya vuli. Kiuzawa, ubabani anatoka kwenye ukoo wenye asili ya kusini ya Makunduchi na Jambiani. Ndoa ya baba mzazi Seif Khatib na mama mzazi Tatu Kombo ilibarikiwa watoto wanne, wanawake wawili na wanaume wawili; Sijamini, Ali, Muhammed (marehemu) na kitindamimba Maimuna (marehemu). Bwana Seif alioa mke mwengine na kubarikiwa mtoto mwanamke aitwaye Rukia (marehemu). Mwandishi huyu ingawa alizaliwa kijijini lakini makuzi yake yalifinyangwa mjini. Alipata elimu yake ya Madrasa katika chuo cha bibi Mwanzena na baadaye kidogo Msikiti Barza. Elimu ya msingi…
Historia ya mtunzi wa ushairi Haji Gora Haji
Haji Gora alizaliwa mwaka 1933 katika Kisiwa cha kale cha kihistoria cha Tumbatu kilichopo Kaskazini ya Unguja. Mwana kindakindaki huyu wa Tumbatu anatoka katika ukoo wa hali duni ya kimaisha watoto sita kwa upande wa mama mmoja na baba mmoja. Anao ndugu wanne wa mama mmoja na baba mbalimbali. Amepata elimu ya madrasa mjini Unguja kwa bibi Mwanadarini katika mtaa wa Vuga. Alimaliza elimu ya Qur’an katika madrasa ya Maalim Ibrahim Juma Ngwali Kisiwani Tumbatu. Mazingira ya kisiwa cha Tumbatu ni ya shughuli za uvuvi na utwesi wa majahazi ya kusafiria. Mapema ya alfajiri ya maisha yake katika umri wa…
Historia ya mwandishi Shafi Adamu Shafi
Ijue historia ya mwandishi nguli wa riwaya za Kiswahili na zilizotafsiriwa kwa lugha za ughaibuni za Kirusi, Kijerumani na Kifaransa ni huyu anayejulikana kwa jina la Shafi wakati wazazi wake walimwita kwa jina la Adam. Tarehe 21 Juni mwaka 1940 ndiyo siku aliyokuja duniani. Uzawa wao wamezaliwa watoto tisa nao ni Saad Shafi, Rukia Shafi, Arafa Shafi (Marehemu), Adam Shafi, Mohammed Shafi, Salma Shafi (Marehemu), Ali Shafi, Zawadi Shafi, na Fatma Shafi. Adam amepitia madrasa na kusoma Kur’ an kabla kupelekwa shule. Kwa Zanzibar katika utoto na ujana wa Adam, elimu ya juu na taaluma ya heshima ilikuwa ni kusomea…
Taasisi ya AU inavyopambana kukuza lugha za Kiafrika
Na Pelagia Daniel Katibu Mtendaji wa ACALAN, Dk Lang Fafa Dampha, hivi karibuni amekutana na Waziri wa Elimu ya Msingi wa Kameruni, Profesa Laurent Serge Etoundi Ngoa, 13 Septemba, 2022. Majadiliano ya viongozi hao yalihusu uteuzi wa muundo wa kitaifa kutumika kama taasisi ya kitaifa ya Chuo cha Lugha cha Kiafrika nchini Kameruni; maendeleo ya sera ya lugha ya taifa, makubaliano ya Utekelezaji ya Dar es Salaam (Assembly Decision) – Kiswahili kama lugha ya kazi ya AU na Lugha ya Mawasiliano mapana Barani Afrika, wiki ya Lugha za Kiafrika, 24 – 30 Januari na lugha za Kiafrika katika mfumo wa…
Siakago kueneza Kiswahili
CHAMA cha Kiswahili katika shule ya upili ya St Albert The Great Siakago Boys kinadhamiria kuboresha matumizi ya Kiswahili miongoni mwa wanafunzi na kupiga jeki shughuli za Idara ya Kiswahili. Aidha, kinakusudia kuwapa wanafunzi majukwaa maridhawa ya kusoma magazeti na kukuza vipaji vyao katika sanaa na fani zinazofungamana na Kiswahili kama vile uigizaji, uanahabari, ulumbi, uandishi wa hadithi na utunzi wa mashairi. Chama hiki ni kiungo muhimu cha Idara ya Kiswahili inayoongozwa kwa sasa na John Macharia Karori ambaye pia ni mlezi wa chama. Wanachama hukutana kila Jumanne jioni kuzamia mada zinazowatatiza katika Kiswahili na kuratibu midahalo na mijadala mbalimbali…
Usanifishaji wa Istilahi
Na Nabil Mahamudu Istilahi ni neno au maneno (msamiati) yanayotumika katika uga fulani maalumu, unaweza ukawa uga wa kimichezo, kitabibu, kisanaa na kiutawala. Idara ya Istilahi na Kamusi katika Baraza la Kiswahili la Taifa ndio yenye kazi ya kukusanya maneno kutoka nyanja mbalimbali ambayo yana uhitaji katika jamii kimatumizi kwa mujibu wa Wema. Msigwa (Mchunguzi wa lugha, Bakita) anabaisha kwamba “kinachofanyika tunakusanya istilahi kutoka lugha mbalimbali huwa mara nyingi tunakusanya istilahi kutoka lugha ya Kiingereza na kuzitafutia visawe, visawe ni yale maneno yanakuwa na maana sawa na msamiati wa lugha ya kiingereza.” alisema Msigwa ambaye pia ni Mkuu wa Idara…
Maoni Mapya