Category: Mashairi
Fahamu mambo muhimu unapochambua mashairi
Yafuatayo ni mambo muhimu unayohitajika kuzingatia kila unapochambua shairi. Muundo/Umbo la shairi Uhuru wa Mshairi Maudhui Dhamira Mtindo wa / Mbinu za Lugha 1. Muundo/Umbo la Ushairi Katika umbo wa shairi, tunaangazia jinsi shairi lilivyoundwa kwa kuangazia mizani, vina, mishororo n.k Aidha, ni muhimu kutaja aina na bahari za shairi zinazohusiana na kila sifa uliyoitaja. Idadi ya mishororo katika kila ubeti – Tumia idadi ya mishororo kubainisha aina ya shairi hilo.Kwa mfano: Shairi lina mishororo minne katika kile ubeti, kwa hivyo ni Tarbia Idadi ya mizani katika kila mshororo na katika kila kipande cha mshororo.Kwa mfano: Kila mshororo una mizani…
HUWEZI KUTIBU MAITI
Assalam allaykum, naisalim jamii,Nasalim binadam, viongozi wa dunia,Salam ya isilam, salama iliyo dua,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Maneno ya aghalabu, na akili za kitume,Sineni yalo ghadhabu, vibaya msiniseme,Kinywa cha kistaarabu, mekuja kutoa shime,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Mwana mwenda mmwele, pitia huku chukule,Mwana wewe mvimbele, kaulilo waambile,Hayafi yalo yalele, ukufi utuzingatile,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Vipi tuchimbe kaburi, maiti tuzifukue?Na tena watanabahari, eti tiba upatie,Maiti haiwi nzuri, ukweli tuupokee,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Kufa wamekufa wengi, tena wakafa kibudu,Jambo liliso msingi, hawakuwa waabudu,ugonjwa wao shilingi, lakini hawakusujudu,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Wagonjwa watazameni, walivyolala wodini,Kama…
Bora nimpe mama
Najaribu ku’dekeza,Japo niwekwe moyoni,Nakupa nisivyoweza,Bado huna shukurani,Huwezi hata kwigiza,Kudhibiti kisirani,Jama jama nimekoma,Kumjali hayawani,Ni heri nimpe mama,Kidogo akithamini. Huishi jibaraguza,Nikupe za benkini,Hukauki Ki’ngereza,“Ai lavi yuu hani,”Pesa ukizimaliza,Huoni yangu thamani,Jama jama nimekoma,Kumjali hayawani,Ni heri nimpe mama,Kidogo akithamini. Yani nikikupa laki,Unataka milioni,Hapo utanidhihaki,Na matusi ya nguoni,“Huwezi kunimiliki,Heri nende kwa fulani,”Jama jama nimekoma,Kumjali hayawani,Ni heri nimpe mama,Kidogo akithamini. Mama’ngu hataki laki,Sikwambii milioni,Baraka hadi zabaki,Nikimpa ishirini,Dua zinatamalaki,“Uishi vyema mjini”,Jama jama nimekoma,Kumjali hayawani,Ni heri nimpe mama,Kidogo akithamini.
KUNISUBU MIYE
Kulalamika niyani, katu sioni ajabu,Ni lalame hadharani, ja abwakaye kalubu,Taoneka mtu duni, kwayo sioni adabu,Wewe miye kunisubu, kunisubu si sononi. Huno wako uraibu, ulio nao mwendani,Maradhi yano kusibu, yamekukaa moyoni,Paza sauti swahibu, wasikie ikhiwani,kunisubu si sononi. wewe miye kunisibu, Najuwa wako undani, wala siwene ajabu,Pendo limekusheheni, pamwe tukiwa karibu,Sitoki mwako kinwani, tuwatanapo ni tabu,Wewe miye kunisibu, kunisubu si sononi. Hako ataye kutibu, zaidi ya Rahamani,Kamwe siwezi jaribu, uipate afuweni,Kila zama ni kitabu, chakwako ni chazamani,kunisubu si sononi. wewe miye kunisubu, Kunisibu kuno ni kwani, yani kuno kunisubu,Umezingwa na sononi, hata unapata tabu,Miye nina kosa gani, ni kwani kujiadhibu,Wewe miye kunisibu,…
NAKUPENDA
Mapenzi yamenishika, kichwa na kiwiliwili,Moyo unanizunguka, nikuwazapo rijali,Ninaandika haraka, nikiwaza mara mbili,Usiku hivi silali, mpenzi nakukumbuka. Saa zimekwenda hasa, mwenzako eti sijali,Simu ninaipapasa, niliyoiweka mbali,Laiti ungenigusa, mapigo katika mwili,Ungejawa na maswali, moyo unavyotikisa. Ai mapenzi hasara, ama ni kitu cha ghali,Mfano nina harara, mwenzako silali kweli,Yananipa ufukara, nisile hata ugali,Nilipo hapa mahali, sio mbali nitagura. Basi ulale unono, uote tupo wawili,Tumeshikana mikono, twendavyo Kila mahali,Ja wayo na kisigino, ya watu hatuyajali,Lala, ulale rijali, hapa ndipo maagano. Mtunzi Filieda SangaMama BMabibo Dsm0753738704
YA WAPI?
YAWAPI leo yawapi, ninaomba kuambiwaNikwache hani kwa lipi, nachelea kuuguwaMwengine katu simpi, apendwae huambiwaYaliyoyakienziwa, zama hizi yakowapi? YAWAPI yale mapenzi, mapenzi yasiovisaApendwae kuyaenzi, akazidisha hamasaMtu siingwe ja nnzi, eti kisa hana pesaSebu mapenzi ya sasa, bora ya enzi na enzi YAWAPI yasioinda, niyafuate yalipoHiyapata nitaganda, simwachi mtu endapoHadi wanivishe sanda, taweka kwake kiapoAendapo nami nipo, simwachii hata nyanda YAWAPI leo mapenzi, ya wawili kupendanaMtu kungiwa simanzi, mpenziwe akinunaNa kujitia kitanzi, pindi wakifarakanaZama hizi sijaona, umejaa upuuzi YAWAPI ninauliza, yale mapenzi asiliYa kucheka na kucheza, wakutanapo wawiliYakijiri ya kukwaza, mkwaza katu halaliHata kama kwa dalili, msiache kunijuza YAWAPI leo mahaba, yaliojaa…
Maoni Mapya