Category: Mashairi
Kama Yale
Nijile kwenu wavyele, mpate kunitambiya,Na ninyi wazungupole, kwenu nataka sikiya,Yalo kuwa siku zile, niyaonayo ni yaya,Kama yale ndiyo haya, yeshakuwa yaleyale. Ni kiza kinizingile, sioni jema na waya,Hawaza hapa na pale, niko katika ruwiya,Naomba mniambile, iniondoke kayaya,Kama yale ndiyo haya, yeshakuwa yaleyale. Nauza kuno ni mbele, ama nyuma niambiya,Si wene niyawazile, niyaonayo mapiya,Usasa ama ukale, pandani nimebakiya,Kama yale ndiyo haya, yeshakuwa yaleyale. Natumbuza wanenile, kwamba zino ndiyo niya,Na vyao vipaumbele, neno litapo timiya,Wametusoza kusile, au hayakuningiya,Kama yale ndiyo haya, yeshakuwa yaleyale. Msambe nina uwele, ugwe mkaja nitiya,Mambo hayendi mile, idhala imeningiya,Kiwa huko ndiyo kule, nimesha potezwa ndiya,Kama yale ndiyo haya,…
Morogoro Nitakuja
Niombacho majaliwa, siku nitajikongoja,Bibi alipozaliwa, kupazuru nina haja,Kitovu kilifukiwa, nyanya alipopataja,Morogoro nitakuja, bibi alipozaliwa. Wakami nawaiteni, wajomba zangu wa haja,Wakutu wa mindukeni, watukuka ninyi waja,Na Mgeta furahini, naja kuleta faraja,Morogoro nitakuja, bibi alipozaliwa. Siku hiyo tajilawa, tarehe sitoitaja,Nisije nikachelewa, kwa kufanya ngojangoja,Kwa mbeta tafurahiwa, Matombo mkiningoja,Morogoro nitakuja, bibi alipozaliwa. Mjomba wangu Mloka, naomba fanya halija,Tambiko ninaitaka, siku nitakayokuja,Tutambikie mizuka, na Kingalu kumtaja,Morogoro nitakuja, bibi alipozaliwa. Babu alipovutiwa, nije waonawambeja,Mke akenda opowa, kwa muhunzi mwenye tija,Binti Fundi akaowa, na babu kuvikwa koja,Morogoro nitakuja, bibi alipozaliwa. Matombo nitapumuwa, japo usiku mmoja,Ngagili naye Mokiwa, niende nao pamoja,Sadaka niende towa, Kolelo kwenye miuja,Morogoro nitakuja,…
Hoja Yangu
Hoja yangu wako wapi, si sarufi kushindana,Meneno huwa situpi, kumbuka nilo yanena,Kule mambo yako vipi, lilo jema kujuzana,Tuambieni bayana, nawauza mko wapi,? Mmeshakuwa wafupi, wenyewe mna pishana,Yenu mapana yawapi, gauni yasio shona,Kweli huwa haichupi, urongo una kazana,Tuambieni bayana, nawauza mko wapi,? Kwenye hili hunikwepi, hapono tutubanana,Mwingine utapitapi, ni hoja iso na mana,Nambiani mko vipi, ya herufi jibu sina,Tuambieni bayana, nawauza mko wapi.? Una izara upupi, thama mwashindwa kunena,Matango yenu yawapi, mlotupa kila kona,Upituzi haulipi, hojani zama kwa kina,Tuamhieni bayana, nawauza mko wapi.? Mie ni nasi si Popi, sijakamilika sanaMakosa niache wapi, vigumu kukosekana,Nikiuzacho muwapi, kwa yale mlo kinena,Tuambieni bayana nawauza…
Yuno Mwambi
Nili nikele pekele, hamuwaza yuno mwambi,Vile ana makelele, na wingi wa jambijambi,Hana nyuma wala mbele, kumbe yu ngali sombombi,Ana kembe yuno mwambi, thama hashiwi kelele. Mwambaji hasa awile, zimetimu tumbitumbi,Hulitumbuza nenole, lisiwe kama uchambi,Wengine liwachokole, kwa maneno ya uchimbiAna kembe yuno mwambi, thama hashiwi kelele. Makaliye nipekule, yana upambaupambi,Latuhadaa umbole, wala si mrume ngambi,Mvuli huwaje vile, na maharimu magombi.Ana kembe yuno mwambi, thama hashiwi kelele. Na yeo niwafunule, yuno mwana chakubimbi,Ndiye asongile ndwele, wakasambaa ja simbi,Akawatusi wavyele, akamba huno ulumbi,Anakembe yuno mwambi, thama hashiwi kelele. Kwa yano niyaonile, hafananile na jimbi,Msongo ummemile, ana haha kila kumbi,Uchao ni yaleyele, kama mpiga…
Wako wapi
Wawapi wale manamba, walio watapitapi,Walo jisifu kuimba, uimbi wao ukupi,Kwa mbwembwe walijigamba, Kwa hojo zilo makapi,Kunuka wala hukwepi, sana sana ukichamba. Sana sana ukichamba, harufu mbi huchupi,Izara itakubamba, kama mvukwa na chupi,Nawauzani wajomba, tambo zenu ziko wapi,Kunuka wala hukwepi, sana sana ukichamba, Mlo kigonga usumba, kwa jina hili mvipi,Urongo mliupamba, tusijue kweli ipi,Cha Siyu kimewakumba, kimbunga ama ni vipi,Kunuka wala hukwepi, sana sana ukichamba, Mambo hayendi kimwamba, hadaa zatoka wapi,Kivambo kimewavamba, ja mwana mpokwa pipi,Mayi huwasoza mamba, seuze ninyi wa pupi,Kunuka wala hakwepi, sana sana ukichamba, Tama navua kiremba, na sefu yangu situpi,Kila mchezea simba, maisha huwa mafupi,Tambeni mlivyo tamba,…
Wanagombea mifupa
Kuna shule kutembea, waliyanenaWala sikutegemea, nilo yaonaMifupa wana gombea, si nyama tena. Kachinjwa ng’ombe mzima, na waungwana,Watu wanaacha nyama, iliyonona,Mifupa wana gombea, si nyama tena. Walaji wakajongea, wa kila konaKimbembe kikatokea, kusukumanaMifupa wana gombea, si nyama tena.
Maoni Mapya