Posted in Mashairi

HUWEZI KUTIBU MAITI

Assalam allaykum, naisalim jamia,Nasalim binadam, viongozi wa dunia,Salam ya isilam, salama iliyo dua,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Maneno ya aghalabu, na akili za kitume,Sineni yalo ghadhabu, vibaya msiniseme,Kinywa cha kistaarabu, mekuja kutoa shime,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Mwana mwenda mmwele, pitia huku chukule,Mwana wewe mvimbele, kaulilo waambile,Hayafi yalo yalele, ukufi utuzingatile,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Vipi tuchimbe kaburi, maiti tuzifukue?Na tena watanabahari, eti tiba upatie,Maiti haiwi nzuri, ukweli tuupokee,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Kufa wamekufa wengi, tena wakafa kibudu,Jambo liliso msingi, hawakuwa waabudu,ugonjwa wao shilingi, lakini hawakusujudu,Kutibu tibu mgonjwa, huwezi tibu maiti. Wagonjwa watazameni, walivyolala wodini,Kama…

Soma zaidi..
Posted in Mashairi

Kasoro ya mkia

Msambe nimechukia, kwa huno wangu uneni,Zanitatiza tabia, walo nazo ikhiwaniZa utu kuwakimbia, na chuki kuwa moyoni,Kumbe nao hayawani, kasoro yao mkia Wanafanana hisia, na akili za kichwani,Sio wa kufikiria, wakaweka akilini,Hata kiwasaidia, hawakumbuki hisani,Kumbe nao hayawani, kasoro yao mkia. Wako ladhi nawambia, wote mungie tabuni,Lengo likose timia, ndipo huwa furahani,Si watu walo timia, wana fanana na Nyani,Kumbe nao hayawani, kasoro yao mkia. Si wandama njema ndia, hila zimewasheheni,Chini chini hupitia, Kusaka wako undani,Walivyo kama shazia, ipenyavyo mkekeni,Kumbe nao hayawani, kasoro yao mkia. Pamoja mtatumia, kiwanacho mfukoni,Sana watakusifia, wana yao mtimani,Kwa ndani wanaumia, ghiliba ipo surani,Kumbe nao hayawani, kasoro yao mkia….

Soma zaidi..
Posted in Mashairi

Mtetezi

Hili natamka wazi, liwe andiko rejea,Nimeichagua kazi, ya lugha kuitetea,Sitakuwa na mbawazi, mtu akiikosea,Nitasimama daima, kutetea kiswahili. Tena pasipo henezi, wala kitu kuchelea,Kukaa kando siwezi, watu wakikionea,Waitwao wachochezi, hovyo wakikinenea,Nitasimama daima, kutetea kiswahili. Bila ya kipingamizi, naapa nitakemea,Maovu na matatizi, lughani yakitokea,Dhahiri lugha azizi, mbali iweze sogea,Nitasimama daima, kutetea kiswahili. Hakika wenye maozi, hili mtajionea,Nitafanya ukombozi, watu nikiwaendea,Pale pakusema jozi, wasije kusema pea,Nitasimama daima, kutetea kiswahili. Tama haya maamuzi, nanyi nawategemea,Tuutumie ujuzi, lugha izidi kumea,Tushikane kama nyuzi, koti tukajishonea,Nitasimama daima, kutetea kiswahili. Mshairi Machinga,mfaumehamisi@gmail.com,+255716541703/752795964,Dar es salaam, Kkoo.

Soma zaidi..
Posted in Mashairi

Mimi nakataa

Kwa kweli ile sauti,mjini ilotangaakwamba tusile chapatipiya nyingine bidhaakwangu ni suala nyeti,na tena ninashangaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe Siachi kula andazi,na chapati za kung’aaunga wala siulizi,nikipewa nitatwaahilo jambo siliweziniache vyakunifaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe Siwezi kuacha kazi,penzi hilo kwangu laawana wakose mavazi,wavalishwe vitambaaniyakose matumizieti ndio ushujaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe Siungi hayo manenokipembeni ninakaanipewe kilo ya nganonijidai kushupaahili siungi mkonohafanyi hata kichaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe Tuzisuse biasharakisa yule kuambaakwangu hii si busarasuseni mie nakaamawazo haya si borayatupwe yana kinyaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe Tamati ya beti sitanawaaga ulamaamimi siachi mafutawala sitoacha mbaahili halikunivutauadui tunazaakisa ni yule jamaamimi mtanisamehe.

Soma zaidi..
Posted in Mashairi

Lisitiri umbo lako

Kakutunuko Jalia, umewashinda wenzako,Tambolo limetimia, kutunza wajibu wako,Una mwendo wa Ngamia, usitiri umbo lako,Watutia hamaniko, umbola ukiachia. Miguu imetimia, ngozi si ya mchubuko,Kuona inavutia, sisemi huo muwako,Ifunike nakwambia, usitiri umbo lako,Watutia hamaniniko, umbolo ukiachia Maozi yametulia, ja mwezi wa mchipuko,Ni raha unapolia, mashavu ya mbonyeko,Tusije kuangalia, ustiri umbo lako,Watutia hamaniko, umbolo ukiachia. Nyoga hebu izuia, uendavyo mwedo wako,Matatani watutia, kwa hiyo mitikisiko,Dhambini tutaingia, usitiri umbo lako,Watutia hamaniko, umbolo ukiachia. Sauti kakujalia, atukuzwe Mola wako,Ni tamu kuisikia, tamu kwa manung’uniko,Nyamaa nakuusia, usitiri umbo lako.Watutia hamaniko, umbolo ukiachia. Rasini hayano tia, yatakwayo kwako yako,Vibaya ukitumia, litakufika anguko,Kwa mwenzawako tulia, usitri umbo lako,Watutia…

Soma zaidi..
Posted in Mashairi

HANYANYASI WANAWAKE

Mume aliye shujaa, mpole mwenye akili,Jandoni aliyekaa, akafunzwa maadili,Anayejuwa sawaa, halali nayo batili,Katu hawezi diriki, kuwapiga wanawake. Mume aliye farisi, mjua moja na mbili,Mwenye mwingi ufanisi, katika lile na hili,Ambaye kwake rahisi, hasira kuzihimili,Katu hawezi diriki, kuwatusi wanawake, Mume aliye mwerevu, anayejua asili,Ambaye unyenyekevu, ni yake kuu adili,Mjua changa na pevu, mume aliye kamili,Katu hawezi diriki, kuonea wanawake. Mume aliye timamu, atazamaye dalili,Subira pia nidhamu, vema amezikabili,Anayejua haramu, yamchukiza Jalali,Katu hawezi diriki, kudhulumu wanawake, Hapa naacha kutunga, sasa nazima kandili,Mume ambaye si bunga, maarifa si kalili,Miko anayeichunga, na mambo kuyajadili,Katu hawezi diriki, kusimanga wanawake, Mshairi Machinga,mfaumehamisi@gmail.com,+255716541703/752795964,Dar es salaam, Kariakoo.

Soma zaidi..