Posted in Matukio ya Kiswahili

Mwana FA asisitiza Watanzania wageukie fursa za Kiswahili kidigitali

Na Mwandishi Wetu Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ametoa wito kwa watumiaji wa Kiswahili kuitazama lugha hii kwa jicho la fursa. Naibu huyo waziri ambaye pia ni alikuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva hapa nchini, amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuwa  wepesi kung’amua kila upenyo kwa lugha hiyo na kuhakikisha inawafaidisha kwa kuwa inatambuliwa, inathaminiwa na kuaminiwa duniani. Mwinjuma ambaye ni maarufu kwa jina la Mwana FA ametoa wito huo juzi Agosti 9, 2023 jijini Mwanza alipofungua Kongamano la sita la Chama cha Lugha na Fasihi ya Kiswahili Tanzania (Chalufakita). Amesisitiza kuwa ni wakati wa kila mtumiaji na…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Waziri Dk Chana kuongoza Kongamano la Kiswahili Mwanza

Saada Amir, Mwananchi Mwanza. Zaidi ya washiriki 150 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajia kukutana jijini Mwanza kwenye kongamano la kimataifa la kujadili hali ya Kiswahili na mustakabadhi wake kwa maendeleo ya jamii na Taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Agosti 7, 2023, Mwenyekiti wa Chama cha Lugha na Fasihi ya Kiswahili Tanzania (Chalufakita), Dk Mussa Hans amesema kongamano hilo litaongozwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Pindi Chana Agosti 9 na 10, 2023 katika hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza. “Mada kuu ya kongamano mwaka huu ni Nafasi ya Kiswahili Kitaifa na Kimataifa na…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Bakita yapongeza Ubalozi wa Marekani kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani

Summary: Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (Unesco) lilitangaza Julai 7 kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili Duniani, mwaka huu ni mara ya pili maadhimisho hayo kufanyika duniani kote. Gadi Solomon, Mwananchi gsolomon@mwananchi.co.tz Dar es Salaam. Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) limeupongeza ubalozi wa Marekani nchini Tanzania kwa juhudi kuhamasisha matumizi ya Kiswahili duniani, huku wakifanya maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani kwa mara ya pili mwaka huu katika ofisi za ubalozi huo jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika maadhimisho hayo ya siku ya Kiswahili yaliyofanyika leo Juni 27, 2023, Katibu Mtendaji wa BAKITA, Consolata…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Ubalozi wa Marekani kuadhimisha Siku ya Kiswahili Duniani Dar

Gadi Solomon, Mwananchi Kwa ufupi: Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (Unesco) lilitangaza Julai 7 kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili Duniani, mwaka huu ni mara ya pili maadhimisho hayo kufanyika duniani kote. Dar es Salaam. Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania unatarajia kufanya maadhimisho ya Kiswahili katika ofisi za ubalozi huo jijini Dar es Salaam leo Juni 27, 2023. Mgeni maalumu katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita), Consolata Mushi. Taarifa iliyotolewa na ubalozi huo, maadhimisho hayo yatayayofanyika kwenye ofisi za ubalozi yanatarajiwa kufanyika kuanzia saa 9 alasiri hadi…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Chaukidu kufanya Kongamano la Kiswahili Arusha

Gadi Solomon, SwahiliHub Dar es Salaam. Chama cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (Chaukidu) kinatarajia kufanya kongamano la Kiswahili Desemba mwaka huu ambalo litafanyika katika Chuo cha Maendeleo na Ushirikiano wa Kimataifa (MSTCDC), Arusha. Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 14-16 Desemba 2023 likitarajiwa kuwakutanisha wadau na wapenzi wa Kiswahili kutoka maeneo mbalimbali. Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti mwenza wa Kamati ya maandalizi hivi karibuni Said Omary, ilisisitiza wapenzi na wana familia ya Kiswahili kuhakikisha wanawasilisha ikisiri zao mapema, ambapo mwisho wa kutuma ikisirikwa ajili ya kongamano hilo ilikuwa Juni 15, 2023. Chaukidu ambayo makao makuu yake yapo nchini Marekani kimekuwa na mashiko…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Maadhimisho ya Kiswahili 2023 kunongeshwa na Swahili Marathon Arusha

Gadi Solomon, Swahili Hub Dar es Salaam. Baraza la Kiswahili la Zanzibar kwa kushirikiana na Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita) wameandaa maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani ambayo mwaka huu kitaifa yatafanyika Zanzibar.Taarifa iliyotolewa na mabaraza hayo imeeleza kwamba maadhimisho ya mwaka huu yatapambwa na mbio za Swahili Marathon ambazo zitafanyika jijini Arusha Julai Mosi mwaka huu.Maadhimisho ya mwaka huu kwa mujibu wa taaarifa hiyo imeeleza kwamba tarehe 4 Julai imetengwa kwa ajili ya Siku ya Wanafunzi wa Sekondari na Shule za Msingi.Vilevile wadau na wapenzi wa Kiswahili watapata nafasi ya kushiriki mdahalo wa wazi utakaofanyika Julai 5.Maadhimisho ya…

Soma zaidi..