Posted in Matukio ya Kiswahili

Makamu wa Rais: Sanaa ikiakisi asili, utamaduni wa Tanzania

Na Nasra Abdallah Pwani. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewahakikishia wasanii Serikali itaendeelea kuwaunga mkono, huku akizitaka sekta za utamaduni, sanaa na michezo kuwanufaisha vijana wengi zaidi nchini. Makamu wa Rais Dk Mpango ametoa kauli hiyo Novemba 11, 2022 wakati akizindua Tamasha la 41 la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni lililofanyika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) mkoani Pwani. “Sanaa ndiyo roho ya taifa lolote, hatuna budi kuhakikisha tuna sanaa yenye asili na maadili yanayotuwakilisha Watanzania.” “Nawasihi Watanzania wenzangu na hasa wasanii wetu wa kizazi kipya kuepuka tabia ya kuiga kila utamaduni bila kuchuja wala kuzingatia maadili yetu,”…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Chakidu yapongeza mabunge ya Afrika Mashariki kukisambaza Kiswahili duniani

Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (Chakidu) kimeandaa kongamano lililofanyika jijini Washington DC, Marekani na kuhuhudhuriwa na wajumbe wapatao takribani 200 kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni. Kongamano hilo lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Havard chini ya uongozi wa Rais wake Prof Leonard Muaka, liliambatana na warsha ya siku moja, mawasilisho ya wajumbe, vikao vya meza mduara na mawasilisho katika ukumbi mzima. Miongoni mwa waliotoa mada elekezi walikuwa ni Prof Maulana Karenga, Prof Alamin Mazrui na Ustadh Abdilatif Abdala huku Balozi wa Tanzania Elsi Kanza akitoa hotuba ya ufunguzi. Siku ya Jumamosi washiriki walipata nafasi ya kuburudika katika ‘Usiku wa Mswahili’ ambapo…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Filamu ya Vuta N’kuvute kuiwakilisha Tanzania tuzo za Oscar

Na Nasra AbdallahDar es Salaam. Filamu ya Vuta N’kuvute imechaguliwa kushindanishwa katika tuzo za filamu za Oscar 2022 zitakazotolewa nchini Marekani Februari mwakani.Vuta N’Kuvute ni filamu iliyotoka mwaka jana imeandaliwa na kampuni ya Kijiweni Production huku mwongozaji wake akiwa ni Amir Shivji. Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa kamati ya kuchagua filamu itakayoshiriki tuzo za Oscar, Dk Mona Mwakalinga, amesema Vuta N’Kuvute imeibuka kidedea kati ya filamu nne zilizowasilishwa kwao kwa ajili ya kwenda kushindanishwa katika tuzo hizo. Amesema kamati hiyo ilifungua dirisha ya kupokea filamu hizo kuanzia Agosti 1 hadi 30, 2022.”Kwa kipindi hicho cha mwezi mmoja kamati…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Mpango ahamasisha matumizi ya Kiswahili kwa Diaspora Marekani

Nabil Mahamudu, SwahiliHub Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania waishio Newyork Marekani, mkutano huo uliaandaliwa na Dk Temba Anesedius ambaye ni mwenyekiti wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Ubalozi wa Tanzania, Marekani. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania waishio Newyork Marekani, mkutano huo uliaandaliwa na Dk Temba Anesedius ambaye ni mwenyekiti wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa Ubalozi wa Tanzania, Marekani. Dk Mpango amewapongeza wanadiaspora kwa jitihada wanazofanya za kuchangia maendeleo katika sekta mbalimbali. Amesema Serikali ya awamu ya sita inatambua mchango wa wanadiaspora…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Kituo cha Utamaduni China chautangaza utamaduni wa Tanzania

Na Gadi Solomon na Pelagia Daniel Dar es Salaam. Kituo cha Utamaduni cha China kilichopo Tanzania, kimepata tuzo kwa mara tatu mfululizo inayotolewa na Kituo cha CCTV Afrika. Tuzo hiyo imekuwa ikihusisha utamaduni majumui wa nchi za Afrika. Vigezo vya ushindani wa tuzo hiyo ulikuwa unawataka watu mbalimbali wanaolezea utamaduni wa jamii yoyote ya Kiafrika na video iliyokuwa imekidhi vigezo iliingia katika ushindani na kujipatia tuzo. Video iliyopata tuzo inaelezea maisha ya msichana wa Kichina Li Huifang anayesoma shahada ya pili ya Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (Tataki). Video iliyowapa ushindi ililenga…

Soma zaidi..
Posted in Matukio ya Kiswahili

Bakita yawapa mbinu Watanzania kunogesha lugha

Gadi Solomon, Mwananchi Dar es Salaam. Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) limewataka Watanzania kuongeza umahiri katika kutumia Kiswahili ili wajitofautishe na watu wanaojifunza lugha hiyo kwa kutumia vinogesho katika mazungumzo, uandishi wa vitabu, mawasilisho, hotuba na tafrija mbalimbali. BAKITA imesema imeweka mkakati ili kuhakikisha Watanzania wanaacha kutumia lugha ya Kiswahili kwa mazoea na maneno yaleyale kila siku. Hatua hiyo ni utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kubidhaishaji Kiswahili kuanzia  mwaka 2021-2031, ikiwa ni pamoja na kusambaza msamiati mpya mara kwa mara. Akizungumza wakati wa kikao cha kumpongeza mdau wa Kiswahili Joramu Nkumbi, Katibu Mtendaji wa BAKITA, Consolata Mushi amesema watumiaji…

Soma zaidi..