Category: Methali
Methali za Kiswahili zilizojaa mafunzo ndani yake
• Damu nzito kuliko maji. • Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe. • Damu ni damu si kitarasa. • Zimwi likujualo halikuli likakumaliza. • Kwendako mema hurudi mema. • Jaza ya ihsani ni ihsani. • Tenda wema uende zako. • Wema hauozi. • Kumpa mwenzio si kutupa. • Usikate kanzu kabla mwana hajazaliwa. • Usihesabu vifaranga kabla hawajaanguliwa. • Dunia ni rangi rangile. • Dunia ni mwendo wa ngisi. • Dunia ni duara huzunguka kama pia. • Dunia ni mti mkavu kiumbe usiuegemee. • Dunia ni tambara bovu. • Jitihada haiondoi kudura. • Jitihada haiondoi amri ya Mungu. • …
Methali za Kiswahili zenye mafunzo utamaduni wa Kiafrika
1. Njia ya siku zote haina alama.2. Nta si asali; nalikuwa nazo si uchunga.3. Nyani haoni kundule, huliona la mwenziwe.4. Njia ya mwongo ni fupi5. Nyimbo mbaya haibembelezewi mtoto.6. Nyimbo ya kufunzwa haikeshi ngoma.7. Nyongeza huenda kwenye chungu.8. Nyota njema huonekana asubuhi.9. Nyumba usiyolala ndani huijui hila yake.10. Nyumba ya udongo haihimili vishindo.11. Nzi kufa juu ya kidonda si haramu. 12. Ondoa dari uwezeke paa.13. Pabaya pako si pema pa mwenzako.14. Padogo pako si pakubwa pa mwenzako.15. Painamapo ndipo painukapo.16. Paka akiondoka, panya hutawala.17. Paka hakubali kulala chali.18. Paka hashibi kwa wali, matilabaye ni panya.19. Paka wa nyumba haingwa.20. Panapo…
Methali 100 zinazotumiwa mara kwa mara na watumiaji wa Kiswahili
1. Ada ya mja hunena, muungwana ni kitendo 2. Adhabu ya kaburi aijua maiti 3. Aibu ya maiti aijua muosha 4. Akiba haiozi 5. Akili ni nywele kila mtu ana zake 6. Akili nyingi huondoa maarifa 7. Alalaye usimuamshe; ukimuamsha, utalala wewe 8. Aliyekando, haangukiwi na mti 9. Asiye kuwapo na lake halipo 10. Asiyefunzwa na mamae, hufunzwa na ulimwengu 11. Asiyejua maana haambiwi maana 12. Asiyekuwepo na lake halipo 13. Asiyesikia la mkuu huona makuu 14. Avumaye baharini ni papa kumbe wengi wapo 15. Baada ya dhiki faraja 16. Baada ya kisa mkasa; baada ya chanzo, kitendo 17. Baba…
Methali tamu za Kiswahili
Methali ni usemi mfupi wa mapokeo wenye mpangilio maalumu wa maneno unaodokeza kwa muhtasari fikra au mafunzo mazito yatokanayo na uzoefu wa maisha ya jamii husika. Ni kauli fupi yenye pande mbili za fikra, ambazo upande wa kwanza huanza upande wa pili humaliza. Tuangalie methali zifuatazo 25; 1. Mali ya bahili huliwa na wadudu. 2. Mama ni mama, hata kama ni rikwama. 3. Mama nipe radhi kuishi na watu kazi. 4. Bandubandu humaliza gogo 5. Manahodha wengi chombo huenda mrama. 6. Maneno matupu hayavunji mfupa. 7. Maneno mazuri humtowa nyoka pangoni. 8. Maneno si mkuki. 9. Mapenzi ni kikohozi, kuyafichika…
Kitanda usichokilalia hukijui kunguni wake
Na Pelagia Daniel Kosa moja haliachishi mke. Kosa moja haliwezi kumhukumu mtu. Methali hii ina maana ya mtu anatakiwa kuwa na subira na ustahimilivu asiwe mtu wa kukasirika au kuhamaki na kukasirika kwa kosa dogo. Kitanda usichokilalia hukijui kunguni wake. Methali hii hutumiwa kuonyesha kuwa ni vigumu mtu kuielewa shida ambayo yeye bado haijamfikia. Lililopita hupishwa. Hutakiwi kujikumbusha mambo yaliyopita au yaliyokupata hasa yale yanayoumiza kwa sababu haitakusaidia zaidi ya kukuumiza na kukurudisha nyuma.
Meno ya mbwa hayaumani
Na Pelagia Daniel Amani haiji ila kwa ncha ya upanga Ukitaka Amani sharti uwe tayari kwa vita. Ikitokea mtu anataka vita au utesi (ugomvi) na wewe atafikiri mara mbili kabla ya kuendelea. Methali hii inatufundisha kwamba, tukitaka tusionewe au tusidhulumiwe, lazima tuwe tayari kujitetea. Hapo ndipo tutakapookoka. Hasira hasara Hasira si jambo zuri mara nyingi huleta hasara tu. Methali hii hutumiwa kuonya watu wasiwe na hasira kwa sababu zinaweza kusababisha hasara ya vitu au uhai wa watu. Meno ya mbwa hayaumani Meno ya mbwa yameumbwa kwa namna ambayo, akifumba mdomo wake, hayaumani kama yanavyoumana yetu sisi binadamu. Methali hii hutumiwa…
Maoni Mapya