Category: Methali
Methali za Kiswahili: Wema hauozi
1. Usishindane na kari; Kari ni mja wa Mungu.2. Usitukane wagema na ulevi ungalipo.3. Usitukane wakunga na uzazi ungalipo.4. Utakosa mtoto na maji ya moto.5. Usiyavuke maji usiyoweza kuyaoga.6. Utaula na chua kwa uvivu wa kuchagua.7. Vita havina macho.8. Vita si lele mama.9. Vita vya panzi, neema ya kunguru10. Waarabu wa pemba, hujuana kwa vilemba11. Wache waseme, mwisho watachoka12. Wafadhilaka wapundaka.13. Wagombanao ndio wapatanao.14. Watu wanahesabu nazi, wewe unahisabu makoroma.15. Wapiganapo tembo wawili ziumiazo ni nyasi.16. Watetea ndizi, mgomba si wao.17. Wazuri hawaishi.18. Wema hauozi..19. Wengi wape.20. Zinguo la mtukutu, ni ufito…
Tujifunze methali hizi 10 na maana zake huru
Usimwamshe aliyelala, utalala wewe. (Katika maisha asiyetaka kuchangamkia jambo zuri na hali analiona usimlazimishe) 2. Usipoziba ufa utajenga ukuta. (Jambo lolote lisipotafutiwa suluhu mapema, likiachwa linaweza kuleta madhara makubwa) 3. Usitukane mkunga na uzazi bado ungalipo. (Usipende kumdharau mtu hujui anaweza kukusaidia wapi) 4. Uso mzuri hauhitaji urembo. (Kitu chochote kizuri kinajidhihirisha chenyewe) 5. Vikombe vinapokaa lazima vigongane. (Popote penye watu Zaidi ya mmoja iwe katika familia au jamii kutofautiana ni jambo la kawaida) 6. Salamu ni nusu ya kuonana. (Salamu au kujuliana hali ni jambo zuri linalowafanya watu kuendelea kuweka ukaribu) 7. Wagombanao ndio wapatanao. (Kutofautiana kimawazo siyo ugomvi,…
Methali ya ‘Ukitaka salama ya dunia, zuia ulimi wako’ imejaa mafunzo
1. Ukienda kwa wenye chongo, fumba lako jicho.2. Ukimpa shubiri huchukua pima.3. Ukimuiga tembo kunya, utapasuka msamba.4. Ukimwamsha aliye lala utalala wewe.5. Ukinyofoa mnofu, ukumbuke kuguguna mfupa.6. Ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kunateketea.7. Ukiona moshi, chini kuna moto.8. Ukiona neno, usiposema neno, hutapatikana na neno.9. Ukiona vinaelea, vimeundwa.10. Ukiona zinduna, na ambari iko nyuma.11. Ukistahi mke ndugu, huzai naye.12. Ukitaja nyoka, shika fimbo mkononi.553. Ukitaka kula nguruwe, chagua aliye nona.14. Ukitaka salama ya dunia, zuia ulimi wako.15. Ukiujua wa mbele, nina ujua wa nyuma.16. Ukupigao ndiyo ukufunzao.557. Ukuukuu wa kamba siyo upya wa ukambaa.18. Ulimi hauna mfupa.19. Ulimi unauma kuliko…
Methali za Kiswahili
1. Aanguaye huanguliwa. 2. Asiye sikia la mkuu, huvunjika guu. 3. Abebwaye hujikaza. 4. Adhabu ya kaburi aijuae maiti. 5. Adui aangukapo, mnyanyue. 6. Adui mpende. 7. Adui wa mtu ni mtu. 8. Afadhali ya Musa kuliko ya Firauna. 9. Ahadi ni deni. 10. Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke. 11. Akiba haiozi. 12. Akili ni mali. 13. Akili ni nywele kila mtu ana zake. 14. Akili nyingi huondoa maarifa. 15. Akutukanae hakuchagulii tusi. 16. Akipenda chongo huita kengeza. 17. Akufaaye kwa dhiki, ndiye rafiki. 18. Akufanyiaye ubaya, mlipe wema. 19. Akupaye kisogo si mwenzio. 20. Akutendaye mtende, mche asiyekutenda. 21. Alisifuye…
Jifunze methali; Jogoo halali na kichwa chake shingoni
Adamu mwenziwe Hawa, mwanamume na mkewe Adui huletwa na kisasi Afadhali ndoa mbaya kuliko ujane mwema Afuatanae na bwana, bwana naye Aibu si kitendo, aibu ni masimulizi Ajaye haulizwi nani, mwache afike Ajizi nyumba ya njaa Akili haba na madaraka makubwa msiba Akili razini ni afya mwilini Akuitaye kajaza ukikawia hupunguza Angenda juu kiboko, makazi yake majini Asiye safari husifu upishi wa mama yake tu Bahati hutaka ujasiri Bahati haiendi kwa kila mtu Bidii ya mchwa hujenga nyumba kwa mate Bila mapenzi dunia hatuiwezi Bora adui mwerevu kuliko rafiki mjinga Bweta la siri ni moyo Chakuota si cha kuiba, cha…
Mpiga ngumi ukuta huumiza mkono
Na Pelagia Daniel Isipowasha hunyeza, methali hii ina maana ya damu ni nzito kuliko maji. Mpiga ngumi ukuta huumiza mkono wake, methali hii hutumiwa kumuonya mtu asishindane na asiyemuweza (mtu mwenye uwezo au nguvu kuliko yeye). Ng’ombe akivunjika guu hukimbilia zizini, ikiwa mtu ameondoka (nyumbani au nchini) kwao au amejitenga na jamaa zake kwa wema au uovu, huko alipokwenda mambo yakaharibika lazima arudi nyumbani.
Maoni Mapya