Jifunze nahau za Kiswahili na mwalimu wa Swahilihub

Gad Solomoni (Mwalimu wa Kiswahili ……BA kiswahili)

simu + 255 712127912

  • Amekuwa popo   – Yu kigeugeu 
    Amevaa miwani   – Amelewa pombe

  • Amekuwa mwalimu     – Yu msemaji sana 

  • Amemwaga unga  – Amefukuzwa kazi

  • Ana ulimu wa upanga    – Ana maneno makali 

  • Ameongezwa unga     – Amepandishwa cheo

  • Agizia risasi    – Piga risasi 

  • Chemsha bongo   – Fikiri kwa makini 

  • Kuchungulia  kaburi   – Kunusurika kifo 
  •  
    Fyata mkia   – Nyamaza

  • Fimbo zimemwota mgongoni    -Ana alama ya mapigo ya Fimbo mgongoni

  • Hamadi kibindoni    – Akiba iliyopo kibindoni

  • Hawapikiki chungu kimoja  -Hawapatani kamwe

  • Kupika majungu     – Kufanya mkutano wa siri

  • Kumpiga [kumvika] kilemba cha ukoka   –  Kumsifu mtu kwa unafiki

  • Kula mlungula   – Kula rushwa

  • Kupelekwa miyomboni  – Kutiwa [kupelekwa] jandoni

  • Kujipalia mkaa      – Kujitia matatani

  • Kumeza [zea] mate     – Kutamani  

  • Kumuuma mtu sikio   – Kumnong’oneza mtu jambo la siri

  • Kumpa nyama ya ulimi   -Kumdanganya mtu kwa maneno matamu

  • Kumchimba mtu    – Kumpeleleza mtu siri yake 

  • Kutia chumvi  katika mazungumzo  –  Kuongea habari za uwongo

  • Vunjika moyo  –  Kata tamaa

  • Yalimkata maini    – Yalimtia uchungu 

  • Kujikosoa    – Kujisahihisha 

  • Kutia utambi  – Kuchochea ugomvi 

  • Kumeza maneno     – Kutunza siri

  • Kula njama     – Kufanya mkutano wa siri

Kumkalia mtu kitako  – Kumsema/kumsengenya

  •  
    Kupiga vijembe  – Kumsema mtu kwa fumbo

  • Kiinua mgongo     – Malipo ya pongezi/uzeeni

  • Kazi ya majungu    – Kazi ya kumpatia mtu posho

  • Kaza kamba     – Usikate tamaa

  • Kumwonyesha mgongo   –  Kujificha

  • Kuona cha mtema kuni    –  Kupata mateso

  • Maneno ya uwani      – Maneno yasiyo na maana/porojo 

  • Mate ya fisi   –  Kata tamaa kupita kiasi

  • Mbiu ya Mgambo    – Tangazo

  • Mungu amemnyooshea kidole   – Mungu amemuadhibu

  • Mkubwa jalala      – Kila  lawama hupitia kwa mkubwa

  • Mkaa jikoni   – Mvivu wa kutembea


Ndege mbaya   – Bahati mbaya


  • Paka mafuta kwa mgongo wa chupa – Danganya

Author: Gadi Solomon