KISWAHILI KWA SHULE ZA SEKONDARI (Kidato cha 1 – IV)

Nahau

NAHAU ZA KISWAHILI

Maelezo mafupi yanatakiwa kukushirikisha katika utajiri mkubwa wa lugha ya Kiswahili katika hadithi, misemo methali, nahau, vitendawili na semi mbalimbali.Hakika hizi ni tunu zenye maarifa, hekima na sanaa iliopo katika jamii ya Waswahili.

Maudhui yaliyomo humu yanalengo l kutumika nyumbani na shuleni. Wazazi, walezi na pia walmu wataweza kutumia fursa zao kuwafunza watoto na vijana kwa kuwajengea wezo na umahiri wa kutumia Kiswahili

Nahau ni nini?

Ni Maneno ya kawaida yenye maana ya uficho ambayo haiendani na maana ya kawaida. Kwa maana nyingine nahau ni Maneno ya kawaida ambayo hayana maana ya kawaida. Kwa mfano iko nahau isemayo”kalia kutu kavu.” Huwezi kupata maana yake kwa kufikiria pekee tu bali kwa kujifunza. Hapa mtu kuwa katika hali ya hatari.

Kwa nini nahau zipo?

Nahau hutumika kutoa ujumbe kwa njia ya uficho. Njia hii hupunguza makala hutoa heshima. Kwa mfano unasema.

“Babu ameaga dunia” Babu amefariki dunia.

“Mjomba ana mkono wa birika” Mjomba ni mchoyo. Angali mifano ya nahau ifuatazo:

1. Acha mkono (Ametuacha mkono)= fariki, kufa,aga dunia.

2. Achiwa mikoba (Fundi John amemwachia mikoba mwanawe wa pili) = Kurithishwa madaraka au majukumu.

3. Bwaga manyanga = Shindwa, kubali kushindwa

4. Changa la macho+uongo, utapeli/danganywa.

5. Veza upatu= Changishana fedha na kupeana kwa zamu

6. Debe shinda= Mtu asiye na uwezo au ujuzi wa jambo fulani.

7. Kaa chonjo= chukua tahadhari, jiepushe na jambo

8. Kaa pwetepwete= legea mwili, kaa kizembe bila kufanya lolote.

9. Kata mbonji= lala usingizi,

10. Kausha/kaushia= nyamazia jambo kwa kujifanya kama hujaona au kusikia jambo.

11. Kutokuwa na kichwa miguu= kukosa mwelekeo au msimamo’

12. Kwa udi na uvumba= Tekeleza jambo ka namna yoyote ile iwezekanavyo

13. Piga jeki= Toa msaada kwa mtu hashspale anapkuwa amekwama (kibiashara au kifedha).

14. Tumbo moto= Hofu, wasiwasi

15. Tupa karata = bahatisha,

16. Piga kitabu= soma sana, soma kwa bidi

17. Vua macho= Tazama kwa makini, sehemu/mahali

18. Vunja mbavu= Chekesha sana

19. Vuta pumzi= Pata mapumziko

20. Weka uzibe= Zuia jambo nyima mtu

21. Zunguka mbuyu/pita mlango wa nyuma= toa rushwa/hongo.

 

Leave a Reply