-
Somo La Kwanza
-
Somo La Pili
-
Somo La Tatu
-
HATUA YA NNE
-
NAHAU ZA KISWAHILI
-
VITENDAWILI
-
METHALI
Vitendawili
VITENDAWILI
Huu ni usemi unaotolewa kwa njia ya fumbo unaoumbwa na pande mbili. Upande mmoja ukiuliza swali na upande wa pili ukijibu swali. Kwa mfano”: ”Popo mbili zavuka mto= macho. Kitendawili hakipigwi wala hakisimuliwi bali hutegwa. Vitendawili hutegwa hivi:
Kutega kitendawili
Mtega kitendawili huanza kwa kusema;
Kitendawili—
Naye msikilizaji huitika
Tega—
Kisha mtegaji kitendawili hukisema kitendawili chenyewe.
- Abeba mishale kila aendako= Nungunungu.
- Aenda mbio ingawa hana miguu =nyoka
- Afahamu sana kuchora lakini hajui achoracho = konokono
4.Amezalia hali, amekufa hali na amerudi hali=Nywele
- Anaota moto kwa mgongo=Chungu kiwapo jikoni.