
- Kwa kweli ile sauti,
mjini ilotangaa
kwamba tusile chapati
piya nyingine bidhaa
kwangu ni suala nyeti,
na tena ninashangaa
kisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe - Siachi kula andazi,
na chapati za kung’aa
unga wala siulizi,
nikipewa nitatwaa
hilo jambo siliwezi
niache vyakunifaa
kisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe - Siwezi kuacha kazi,
penzi hilo kwangu laa
wana wakose mavazi,
wavalishwe vitambaa
niyakose matumizi
eti ndio ushujaakisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe - Siungi hayo maneno
kipembeni ninakaa
nipewe kilo ya ngano
nijidai kushupaa
hili siungi mkono
hafanyi hata kichaa
kisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe - Tuzisuse biashara
kisa yule kuambaa
kwangu hii si busara
suseni mie nakaa
mawazo haya si bora
yatupwe yana kinyaa
kisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe - Tamati ya beti sita
nawaaga ulamaa
mimi siachi mafuta
wala sitoacha mbaa
hili halikunivuta
uadui tunazaa
kisa ni yule jamaa
mimi mtanisamehe.
Maoni Mapya