Muuaji Asakwe-5

Baada ya kumaliza kuhakikisha hakuna mtu aliyemwona, ndipo John Bosho alipolitia moto gari lake na kuliondoa kwa mwendo wa taratibu, kuliingiza katika barabara kuu, kuelekea Tabata Mawenzi, nyumbani kwa Anita kutimiza azma yake ya kuuondoa uhai wake! Akiwa ndani ya gari huku akiendesha kwa mwendo wa wastani, alichomoa simu yake ya mkononi na kumpigia Anita kumtaarifu kuwa anakwenda hapo nyumbani kwake.

Simu ikaanza kuita!

********         

MAJIRA ya saa nane za mchana, Anita alikuwepo nyumbani kwake, Tabata Mawenzi. Wakati huo ndiyo alikuwa amepumzika kwenye sofa sebuleni, huku akiwa na mawazo mengi sana. Tokea akorofishane na mchumba wake, John Bosho, alikuwa hana raha kabisa, na alikuwa anapanga kurudisha nyumba na kuondoka haraka sana!

Simu ya mkononi iliyokuwa juu ya meza ndogo ya kahawa hapo sebuleni, umbali mfupi tu na aliokuwa amekaa kwenye sofa, ilianza kuita. Akanyanyuka kivivu na kuichukua, akiwa na hamu ya kutaka kujua mpigaji wa simu hiyo, hasa ukizingatia siku ile hakuwa katika hali nzuri kabisa, alihitaji kupumzika.

Lakini Anita alipoangalia namba za mpigaji wa simu hiyo, aliona ni ya siri isiyoonyesha namba ya mpigaji kwa tarakimu, akaduwaa kwanza, halafu akaipokea kwa sauti ndogo, “Anita anaongea…”

“Oh. hujambo mpenzi wangu?” Upande wa pili wa simu ukasema kwa sauti nzito, ambayo siyo ya mtu mwingine zaidi ya John Bosho, mchumba wake waliokorofishana. Na wakati huo ndiyo alikuwa ndani ya gari lake, akielekea nyumbani kwa Ania katika kutekeleza adhabu yake aliyokuwa amempangia!

“Si…sijambo…” Anita akaitikia kwa kusita kidogo mara baada ya kuitambua sauti ya huyo mpigaji wa simu hiyo!

“Ni mimi mchumba wako, John Bosho…” John Bosho akajitambulisha kwani alijua kuwa namba haikusomeka kwenye kioo cha simu.

“Nimeshajua ni wewe John…unasemaje?” Anita akauliza kwa hasira!

 “Vipi tena?” John Bosho akauliza. “Mbona unakuwa mkali mpenzi Anita?”

“Mimi siyo mpenzi wako, John …naomba unisahau na usinijue!”

“Usifanye hivyo…naomba tukutane ili tuweze kulitatua tatizo hili…”  John Bosho akaendelea kumsihi Anita.

“Haiwezekani, sitaki kuonana na wewe kabisa!” Anita akamwambia na kukata ile simu, huku akifyonza kwa nguvu!

Baada ya kuikata ile simu, Anita akaiweka mezani na kuendelea kuwaza. Hata hivyo ile simu ikaita tena, mpigaji akiwa ni mtu yule yule mchumba wake, John Bosho! Hivyo akaamua kumsikiliza ingawa ilikuwa kero kwa upande wake!

“Unasemaje? Mimi naona kama unanisumbua!”

“Naomba uwe mtulivu Anita. Daima mvumilivu hula mbivu…” John akaendelea kumwambia Anita.

“Sikiliza John. Natumaini wewe ni mtu mwelewa sana! Siwezi kuwa mtulivu…si unajua kwamba umeamua kunisaliti kwa penzi la rafiki yangu Getruda? Basi endelea naye na mimi uniache nilivyo!” Anita akamwambia kwa sauti iliyojaa uchungu mwingi!

“Ok, hayo tuyaache…mimi nitakutembelea hapo nyumbani jioni ya leo ili tuyamalize. Mbona ni mambo madogo sana?”

“Wewe unaona haya ni mambo madogo? Hapana, naomba usije John…” Anita akaendelea kumwambia!

“Sasa nisikilize kwa makini sana Anita,” John Bosho akamwambia na kuendelea. “Mimi nitakuja hapo nyumbani upende usipende. Hakuna mtu asiyejua kuwa mimi ni mmoja wa wahusika wa hapo. Nafikiri unanijua kwamba mimi ni mtu wa aina gani! Ukicheza nakuondoa uhai wako mara moja!”

“Oh, Mungu wangu!”

“Mwombe sana huyo Mungu wako!” John akamaliza kusema!

Simu ikakatwa!

Anita akavuta pumzi ndefu na kuzishusha, halafu akajiegemeza kwenye sofa huku mawazo yake yakiwa mbali. Hakujua John Bosho alikuwa anahitaji kitu gani kutoka kwake, wakati alishamwambia kuwa hataki uchumba tena, na pete yake alikuwa ameshamvulia na kumrudishia!

Anita aliiangalia saa yake, ambayo ilionyesha imetimu saa nane mchana, hivyo hakuwa na jingine zaidi ya kuingia chumbani ili kupumzika chakula kiteremke. Baada ya kujilaza tu, alipitiwa na usingizi mzito uliochanganyika na mawazo aliyokuwa anawaza, na pia jinsi John alivyomchanganya!

Anita alianza kuota ndoto za kutisha, huku akikumbwa na majinamizi, ikiwa ni ndoto ambayo alikuwa hajawahi kuota hata siku moja, ikiashiria ni ndoto ya kifo! Ndani ya usingizi huo, aliota akijiona anaruka angani kwa kasi, akiyapita mabonde na milima mikubwa, ambayo aliweza kuiona kwa chini. Hatimaye akaenda kutua juu ya mlima mmoja mrefu uliotengenishwa na bonde lenye kina kirefu ajabu.

Kwa mbele nako aliuona mlima mwingine mrefu kama ule aliokuwa amesimama yeye, ambao uliwatengenisha kwa lile bonde. Mara muungurumo kama wa radi ulitokea na kulipuka katika mlima ule wa pili, ambapo alitokea mtu mmoja aliyekuwa amevalia mavazi meupe yanayong’aa. Mtu yule akanyoosha mkono wake wa kulia na kusema kwa sauti iliyokuwa inatoka kwa mwangwi uliotetemesha!

“Anitaaa….aaaa!”

“Beeee!” Anita akaitikia kwa hofu!

“Wewe mwanadamu…nakukaribisha huku kwetu!” Mtu yule akaendelea kumwambia!

“Hivi huku ni wapi?” Anita akauliza huku akiwa na wasiwasi mkubwa.

“Nilisikilize kwa makini wewe mwanadamu. Huku ni peponi!”

“Lakini mimi siwezi kufika huko mpaka nivuke bonde hili!”

“Ni kweli huwezi kuvuka katika bonde hili!” Mtu huyo akamwambia na kuongeza. “Unahitaji kutubu dhambi zako…na ukitubu tutakukaribisha!”

“Oh, basi nitatubu ili  niweze kuvuka…”

“Nasikitika sana mwanadamu! Umechelewa…huu siyo muda wake!”

“Oh, Mungu wangu! Kwa nini?”

“Napenda kukutaarifu ujiandae…Muda siyo mrefu utakuja huku. Lakini hutanifikia katika himaya hii ya peponi.!”

“Sitafanikiwa?” Anita akauliza. “Isipokuwa?”

“Ni lazima utazama ndani ya bonde hili!”

“Kwa nini nizame?”

“Utazama kwa ajili ya dhambi zako zilizotukuka!”

“Mamaaa..aaa!” Anita akalia kwa kupiga ukulele mkubwa! Ni ukulele ambao ulitoa mwangwi ulioenea kote!

“Haya, jiandae kuja huku! Karibu sana katika himaya ya peponi” Mtu huyo akamwambia huku akimnyooshea kidole!

Muungurumo mkubwa ukatokea! Mtu huyo akazama katika mawingu meupe yaliyokuwa yametanda angani!

“Ooohps!” Anita akapiga yowe kubwa na kushtuka katika usingizi ule wa mchana!

Anita akayafikicha macho yake na kuona kuwa alikuwa ndani ya chumba chake, ambapo alikuwa amelala siyo muda mrefu. Hatimaye baada ya kugundua kuwa alikuwa chumbani mwake, akashuka kitandani na kukaa huku akitafakari ndoto ile. Ukweli ni mkwamba ilikuwa inatisha ilikuwa inatisha!

Je, iliashiria kitu gani?

Hivyo basi, Anita akanyanyuka kutoka pale  kitandani. Halafu akachukua taulo lililokuwa limetundikwa, pamoja na upande wa kitenge, ambao alijifunga na kuamua kwenda kujimwagia maji ndani ya bafu lililokuwa mle ndani, ili kuondoa uchovu uliotokana na usingizi wa mchana.

        ********   

John Bosho alisimamisha gari lake katika uwanja mdogo uliokuwa mbele ya maegesho ya kuegesha magari, jirani na Mawenzi Bar, eneo la Tabata Mawenzi. Sehemu hiyo iliyokuwa na miti ya muarobaini iliyokuwa na kivuli, pia, palikuwa na magari mengine kama matatu hivi yaliyokuwa yamepaki hapo, hivyo yeye akalipaki la kwake katikati ya hayo magari.

Majira hayo ya saa tisa za alasiri, jua lilikuwa bado ni kali, kiasi cha kuleta kero kwa watembea kwa miguu na wasafiri wanaotumia mabasi ya daladala, ambao wengine walijificha katika vivuli vya miti. Baada ya kupaki lile gari, John akashuka na kuufunga mlango wa gari huku akihakikisha kama ameufunga vizuri, halafu akaondoka kwa mwendo wa taratibu kuufuata uchochoro mmoja uliotenganisha nyumba na nyumba.

John Bosho alitembea kwa mwendo wa kawaida tu, huku katika mkononiwake wa kushoto ameshika bahasha ndogo iliyokuwa na kitu muhimu, bomba moja la sindano lililokuwa na sumu kali ndani yake, ambayo ni ya kumshughulikia mchumba wake, Anita. Hivyo akaendelea kuufuata ule uchochoro na kutokea kwenye eneo hilo lililokuwa liimezungukwa na uzio wa ukuta uliojengwa kwa matofali. Ndani yake ndipo palipokuwa na nyumba kama tano hivi, ambapo nyumba aliyopanga Anita ilikuwa moja wapo.

Pale John akasimama kwa muda huku akichungulia ndani kwa kutumia matundu madogo yaliyokuwa katika ukuta, ambayo yalitengenezwa kama urembo, na pia kuwezesha upepo kuingia ndani, lakini hakuona mtu yeyote, aliyekuwa pale uani. Palikuwa kimya kabisa, na kitu alichoweza kuona, ni bustani ya maua na miti iliyokuwa pale.

Basi, ndani ya nyumba moja wapo, ambayo haikuwa mbali na uzio wa ukuta, ambapo pia siyo mbali na hapo alipokuwa amesimama nje ya ukuta,  ndipo alipokuwa anaishi Anita, mchumba wake. Vilevile, wakati huo alikuwepo ndani kwake, ikiwa ni muda mfupi tu tokea amempigia simu na kumjulisha kuwa yeye atakuwa mgeni wake, ingawa alikataa.

Hapo alipokuwa amesimama John Bosho, palikuwa na miti ya muarobaini iliyofungamana. Hivyo hakupoteza muda, akauruka ule uzio kiufundi bila kuonekana na mtu yeyote hadi alipoibukia ndani ya ua wa nyumba hiyo, umbali mfupi kutoka katika nyumba anayoishi Anita. Baada ya kuingia, akajibanza kwenye kona moja iliyokuwa na maua yaliyofungamana, tayari kulivizia windo lake, mchumba wake, Anita!

Ni kwamba John Bosho alikuwa amepanga aingie mle ndani ya nyumba ya Anita bila kuonekana na mtu yeyote, ili amfungie kazi, ukizingatia alifika pale kwa kazi moja tu ya kuua, na si vinginevyo! Hivyo akaendelea kubanisha pale kwenye kivuli cha maua ili kuvuta subira mpaka atakapomwingilia mle ndani kwake kwa kupitia katika mlango mkubwa aliokuwa anauangalia kwa makini! 

Baada ya kuhakikisha kila kitu kilikuwa shwari pale uani, John Bosho alijitoa pale mafichoni na kuuendea mlango ule wa kuingia ndani ya nyumba ya Anita. Baada ya kuufika, akaufungua taratibu na kuingia ndani huku akinyata. Akaanza kumtafuta Anita kila kona, hadi alipogundua kuwa alikuwa ameingia bafuni kuoga na kuufunga mlango bila komeo, kwa vile ilikuwa ni ndani kwake, na alikuwa peke yake.

John Bosho aliuendea mlango ule wa bafuni, ambao pia aliufungua taratibu, ambapo pia aliweza kumwona Anita akiuvua ule upande wa kitenge aliokuwa amejifunga pamoja na taulo, na vyote kuvitundika kwenye kamba iliyokuwa mle ndani. Akabaki uchi na kujiandaa kujimwagia maji bila kujua kuwa kuna mtu aliyekuwa anamwinda pale mlangoni!

        ********

MARA baada ya Anita kuvua kienge na kubakia uchi kama alivyozaliwa, na kabla hajajimwagia maji, alijiangalia takriban dakika moja hivi, na kujiona alivyokuwa na umbile zuri na la kuoendeza. Hapohapo akajiuliza, imekuwaje John Bosho, mchumba wake, amkinai na kumkimbilia Getruda rafiki yake? Ni kitu gani alichokosa mwilini mwake?

Hata hivyo, Anita akayatupilia mbali mawazo hayo, halafu akaliangalia bomba la mvua lililokuwa juu, ambalo alikuwa tayari kulifungua ili aanze kujimwagia maji. Lakini kabla hajafanya lolote, akashtukia akirukiwa na kiumbe chenye nguvu mithili ya mnyama,  Simba, na kiumbe hicho kikamng’ang’ania maungoni mwake!

Anita alichanganyikiwa kwa kitendo hicho kilichotokea ghafla kana kwamba alikuwa ndotoni, na kutaka kupiga kelele za kuomba msaada. Hata hivyo sauti yake haikuweza kutoka, kwani alizibwa mdomo na mkono wenye nguvu nyingi!

“Oooohpsi!” Anita akapiga kelele ambayo haikuweza kusikika mbali kwa vile alikuwa amezibwa mdomo!

“Tulia!” John Bosho akamwambia kwa sauti ndogo lakini nzito!

“Ooh! Unataka nini?” Anita akamuuliza!

“Ni mimi John Bosho!” Akamwambia kwa sauti kavu na kuendelea “Nimekuja kama nilivyokwambia muda siyo mrefu kwenye simu! Hivyo nakusihi utulie kimya kabla sijakumaliza!”

“Oohps….Ooohps!” Anita akatoa sauti baada ya mdomo wake kuachiwa na John aliyekuwa amemziba kwa mkono wenye misuli!

“Nakuonya tena! Tulia!” John Bosho akaendelea kumwambia huku akimwonyesha bastola aliyokuwa ameikamata mkononi!

“Oh, umepitia wapi mwanaume wewe?” Anita akamuuliza huku bado wasiwasi mwingi umemjaa!

“Unashangaa? Nimepitia mlangoni!” John Bosho akaendelea kusema huku amekunja uso wake! Ni uso uliokuwa unatisha mithili ya jitu la porini!

“Mbona unanifuata sana?” Anita akamuuliza huku akiwa na wasiwasi!

“Ni kama nilivyokwambia mwanzo Anita!..” John Bosho akamwambia huku akimwangalia kwa uchu wa ngono, ukizingatia alikuwa na umbile zuri la kike lenye kutamanisha! Halafu akamvutia kwake na kutaka kumkumbatia!

“Tafadhali toka, usiniguse!” Anita akamwambia huku akikunja uso wake!

“Lazima nikuguse mpenzi!”

“Nitakupigia kelele!” Anita akasema huku akimsukuma John Bosho.

“Huwezi kupiga kelele, naomba uwe mtulivu, na kutulia kwako ndiyo usalama wa maisha yako!” John akamwambia Anita huku akimfuata!

“Unataka kufanya nini?”

“Nataka nikufanye kwanza, halafu adhabu nyingine ifuate baadaye!”

“Ooohpsi!” Anita akapiga ukelele mdogo!

“Usiniwangie mchana!” John Bosho akamwambia Anita. Halafu akamkamata kwa nguvu na kumwangusha chini sakafuni!

Kwa vile Anita alikuwa uchi wa mnyama, uchu wa ngono ukaendelea kumwandama John Bosho, na baada ya kumwangusha chini, akafungua zipu ya suruali yake na kutoa ‘dhakari’ yake. Akaanza kumbaka  Anita mbaye kwa muda ule hakuwa na nguvu yoyote baada ya John kumbana kwa nguvu pale sakafuni hadi alipomaliza haja yake huku akichekelea!

Ni unyama wa kutisha!

Alipomaliza kumbaka Anita, John Bosho akampiga kofi moja la nguvu lililomfanya achanganyikiwe na kuona nyota nyota! Halafu bila kupoteza, akachukua ile bahasha ndogo aliyokuwa nayo, na ndani yake kulikuwa na bomba la sindano, lililokuwa na sumu kali aliyokuwa ameitayarisha kwa ajili ya kazi ile. Akamchoma Anita na sumu yote ikamwingia mwilini mwake!

Baada ya John kumaliza kumchoma ile sindano, akalichomoa lile bomba na kulitia ndani ya ile bahasha, ambayo aliiacha kando ya mwili wa Anita uliokuwa umelala pale kwenye sakafu ya bafuni. John akasimama kwa muda huku akiuangalia ule mwili mwororo wa Anita, ambao muda siyo mrefu alikuwa akijiburudisha juu yake. Akatikisa kichwa kwa uamuzi ule alioamua kumfanyia mwanadada huyo, ambaye kamwe hakupaswa kupewa adhabu kama ile ya kinyama!

Kwa upande wa John, aliamua kumuua Anita kwa kutumia njia ya sumu, kwani hakupenda kutumia bastola ingawa alikuwa nayo muda wote. Sumu ile ikaendelea kuingia na kusambaa katika mwili wa Anita na kumfanya apate maumivu makali sana huku nguvu zikimwishia na kuona giza!

“Ooohpss!” Anita akendelea kupiga kelele!

“Utakoma kuringa!” John Bosho akaendelea kumsimanga!

“Oh, unaniua John…oh!”                         

“Sikuwa na jinsi…siri zangu nyingi unazijua! Hivyo huna budi kufa!”

“Oh, Mungu wangu!” Anita akaendelea kusema huku akifumba macho!

“Kwa heri Anita…kawasalimie kuzimu!” John Bosho akamwambia huku akijiandaa kuondoka.

“Mungu atalipa…” Anita akamaliza kusema huku roho ikianza kuachana na mwili!

Baada ya kuhakikisha Anita amekufa, John Bosho akatoka  mle ndani ya bafu lile kwa njia ileile aliyoingia nayo, hadi alipofika nje. Halafu akatoka nje kabisa wa nyumba ile, kwa kuuruka ukuta ule wa upande wa nyuma na kutokomea kuufuata ule uchochoro hadi sehemu ile aliyokuwa amepaki gari lake. Hakuna mtu yeyote aliyemshtukia kuhusiana na mauaji yale aliyofanya, na alipolifikia gari lake akapanda na kuondoka eneo lile haraka sana akiwa na matumaini!

Baada ya kufika mbali na eneo lile la tukio, akiwa ndani ya gari lake, ndipo John Bosho alimpigia simu Getruda, na kumjulisha kuwa alishamaliza kazi ya kumuua mchumba wake, Anita!

“Haloo…John…” Getruda akasema.

“Ndiyo Getu…” John Bosho naye akasema.

“Unasemaje?”

“Nakujulisha kwa mimi ndiyo nimetoka kummaliza Anita!”

“Umemuua?”

“Ndiyo!”

“Oh, Mungu wangu!”

“Ni kama nilivyokuwa nimepanga! Sasa nakuonya kwamba usije ukatoa siri hiyo! Hakuna aliyeona!”

“Oh, siwezi kusema…”

“Haya kwaheri!” John Bosho akasema na kukata simu!

Upande wa pili alipokuwa Getruda, alibaki ameing’ang’ania simu yake mkononi! Alikuwa amechanganyikiwa sana, yaani amemuua mchumba wake Anita?

Hakuamini!

*******

KELELE za kuomba msaada ndizo zilizowashtua majirani waliokuwa wanaishi katika nyumba nne zilizokuwa mle ndani ya uzio alipokuwa anaishi Anita, ambao walikuwa vyumbani mwao, pamoja na majirani wengine wanaozizunguka nyumba hizo zilizojengwa kwa mtindo wa kupendeza ndani ya uzio madhubuti.

Ni kelele ambazo Anita alipiga pale mwanzoni wakati John Bosho alipokuwa akimdhibiti kule ndani kwake, bafuni, katika kutaka kumtoa roho yake. Hakika ni kelele zilisikika kama mtu aliyekuwa anakoroma kwa kubanwa pumzi. Majirani walitoka vyumbani mwao haraka haraka, ndani ya zile nyumba nyingine ziliyokuwa jirani na anayoishi.

Majirani hao walikuwa pamoja na mama mwenye nyumba aliyopanga Anita, Bi. Debora Mjema, ambaye naye alikuwa anaishi humohumo katika moja ya nyumba hizo tano. Halafu wakaelekea ndani ya nyumba hiyo aliyopanga, iliyokuwa hatua chache, ambapo kelele zile zilitokea. Baada ya kufika pale nje, walikuta ule mlango mkubwa umefungwa kwa ndani bila komeo.

Haraka wakaufungua mlango ili kujua kilichokuwa kimemsibu mwanadada Anita, na kumfanya apige makelele ya kuomba msaada. Hatimaye majirani wawili walifanikiwa kuingia mle ndani ya bafu alilokuwa anaoga. Wote walikuwa ni wa wanaume, ambao baada ya kuingia walishangaa kuukuta mwili wa Anita ukiwa umelala sakafuni umetulia kimya, tena ukiwa uchi wa mnyama!

Mwili huo wa Anita uliokuwa bado umelala pale sakafuni, ulionyesha dalili zote kwamba alikuwa ameshakata roho muda mrefu! Michirizi ya damu ilionekana ikichuruzika kutoka mdomoni na puani, kiasi cha kuwafanya wale wanaume wawili watoke nje mbio, hadi walipofika sebuleni!

“Kuna nini jamani?” Mtu mmoja akauliza kati ya wale majirani.

“Mh, hatari!” Akajibu mmoja wa watu wawili waliotoka mle bafuni kuangalia!

“Hatari ya nini?”

“Tumemkuta Anita amelala sakafuni,” mtu mwingine akasema na kuongeza. “Tena yuko uchi!”

“Amefanya nini sasa?” Akaendelea kuuliza kijana mwingine aliyetaka kujua kilichojiri.

“Bila shaka amepata matatizo mazito!” Mwanaume huyo aliyetoka mle bafuni akasema.

“Jamani, akina mama ingieni mumvishe hata upande wa khanga!”

“Ooohpsi!” Akina mama wakapiga kelele baada ya kujua kuwa mambo yalikuwa yameshaharibika!

Mara baada ya kusema vile, akina mama wawili waliokuwa pale waliingia mle ndani ya bafu. Baada ya kuingia humo bafuni, waliukua mwili wa Anita ukiwa umelala uchi pale sakafuni. Haraka wakatoa upande a kitenge na kuufunika vizuri mwili huo, na hatimaye wakatoka mle bafuni na kujiunga na watu wengine, akiwemo mama mwenye nyumba, ambao walikaa na kutafakari cha kufanya.

Kwa vile mwili huo wa Anita haukuonyesha uhai wowote,  ndipo ilipojulikana kwamba alikuwa ameshakufa! Watu wengi walianza kukusanyika wakiwemo majirani na wapita njia waliofika kushuhudia tukio lile la kutisha jioni hiyo, kila mmoja akitokwa na machozi ya uchungu kwa kushindwa kuvumilia!

Vilionekana vikundi kadhaa vya watu waliokuwa wakiongea hili na lile. Hata hivyo hawakujua ni mtu gani aliyesababisha kifo hicho cha kutatanisha! Simu ya dharura ikapigwa na mmoja wa mashuhuda, ili kuwajulisha Jeshi la Polisi juu ya tukio hilo la kifo cha mwanadada, Anita Anthony.

Author: Gadi Solomon