-
Mbunge alivyopiga Kiingereza na kuwaacha wenzakke hoi "Kimakonde hicho"
Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kusini Ally Kasinge siku ya Jumatatu Februari 6,2023 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa Februari mwaka 2022 hadi Januari mwaka 2023. -
Mbunge Getere aharibu hali ya hewa Bungeni "Hakuna haja ya kudanganyana nashindwa kuelewa"
Mbunge wa Jimbo la Bunda vijijini, Boniphace Mwita Getere Jumatatu Februari 6,2023 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa Februari mwaka 2022 hadi Januari mwaka 2023. -
"Tuwe wakweli, hakuna punguzo la mafuta" Mbunge chumi ailipua serikali
Mbunge wa Mafinga Mjini, Kosato Chumi siku ya Jumatatu Februari 6,2023 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa Februari mwaka 2022 hadi Januari mwaka 2023. -
Mbunge Shally Raymond afunguka mazito Bungeni
Mbunge Shally leo Jumatatu Februari 6,2023 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa Februari mwaka 2022 hadi Januari mwaka 2023. -
"Aliwatia umasikini wavuvi wa nchi hii" Waziri Bashe ampiga vijembe Luhaga Mpina
Vita ya maneno kati ya mbunge wa Kisesa na Waziri wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba bado ni mbichi ambapo leo Jumatatu Februari 6,2023 Mpina amemchokonoa tena Dk Mwigulu sasa akitaka akiomba bunge lipitishe Azimio la kuitaka Serikali kupeleka bungeni taarifa ya matumizi ya fedha zilizokopwa nje ya bajeti lakini akipendekeza Waziri wa Fedha awajibike.
Akochangia leo katika taarifa ya Kamati ya Bajeti, mbunge huyo amesema Kuna kusuasua katika usimamizi wa matumizi ya fedha ndiyo maana kumekuwa na malimbikizo ya deni la Taifa ambalo litapelekea riba kubwa kwa siku za usoni na hivyo kuongeza mfumuko wa bei.
Kuhusu mbolea amesema kumekuwa na udanganyifu ndani yake na akaomba pia jambo hilo kupelekwa bungeni likajadiliwe kwa mapana.
Akijibu kuhusu suala la mbolea, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe Serikali itaendelea kutoa ruzuku ya mbolea kwani katika awamu hii suala la ufuatiliaji ni mkubwa kuliko Serikali zikizotangulia. -
DC Msando awataka wanaume wasiogope kupimwa Tezi dume
Wanaume wameshauriwa kujitokeza mapema kupima ugonjwa wa tezi dume katika hospitali kwani vipimo vinavyotumika ni rafiki na havina tatizo kwao,ili kuweza kupatiwa matibabu.
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga Albert Msando,wakati akihitimisha wiki ya kampeni ya Marafiki wa Maendeleo Handeni,(MMAHA) na kusema kuwa wanawake ndio hujitokeza sana,hivyo wanaume nao wasibaki nyuma -
Lissu apokewa kijijini kwao aonyesha makovu , namna alivyopigwa risasi// ndugu wasikitika
Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara, Tundu Lissu leo Jumatatu Februari 6, 2023 amepokelewa rasmi nyumbani kwao, katika Kijiji cha Mhambwe, Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida.
Lissu aliondoka nchini usiku wa Septemba 7, 2017 kupekekwa Nairobi nchini Kenya kwa matibabu, baada ya mchana wa siku hiyo kushambuliwa kwa risasi akiwa nyumbani kwake Area D, jijini Dodoma.
Lissu ambaye amerudi rasmi nchini baada ya kuishi uhamishoni kwa takriban miaka saba, ambapo hajawahi kufika nyumbani kwao na mara baada ya kuwasili amepokewa kimila.
Baada ya kufika eneo la nyumbani kwao, amesimama nje ya uzio wa (nje ya boma) makazi yao na wanafamilia wakiwamo shangazi na bibi zake walifanya Misa pamoja na kuomba Dua kwa kuwa familia yake ina Waislamu na Wakristo na baadaye walifanya maombi ya kimila.
Shangazi na bibi zake walimwagia maji ya baraka ya kimila kwa lengo la kumtakasa kabla ya kuingia ndani ikiwa na lengo la kuondoa mikosi kutokana na yaliyomkuta.
Mpwa wa Tundu Lissu, Liku Kilindo amesema imekuwa ni siku ya furaha kwa kuwa wanafamilia takriban 100 walikusanyika kwa ajili ya kumpokea mtoto wao ambaye amewaonyesha makovu ya risasi.
Amesema licha ya furaha waliokuwa nayo hapo kijijini kwao Mahambe, Lissu ameielezea familia jinsi alivyoshambuliwa, sababu za kuondoka tena mwaka 2020 na sababu za kurejea nyumbani. -
Waziri Mwigulu ajibu Mapigo kwa Mpina "dokta yangu siyo ya kupewa nimeisomea darasani" afunguka
Waziri wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba amesema ni kazi kubwa kumfundisha mtu yuleyule ambaye hataki kuelewa lakini dokta yangu siyo ya kupewa bali nimeisomea darasani,"
Waziri huyo amesema hakuna shaka Tanzania bado iko salama na suala la kushuka kwa akiba ya fedha amekiri kubwa zimeshuka kwa sababu fedha nyingi zimwingia kwenye miradi mikubwa ya maendeleo.
Hata hivyo Dk Mwigulu amesema uchumi ni sayansi hivyo unahitaki wajuzi katika uchangia na kuomba wanaoongoza bunge kuwa makini kuhusu hoja za baadhi ya wabunge Kwa madai wanaweza kuwa wapitishaji wa dili za watu. -
Kutoka Ikungi "Tufanye Siasa za kistaarabu, situkani mtu" Mbunge Kingu aionya Chadema
Wakati Mikutano ya kisiasa ikiruhusiwa huku tukishuhudia mikutano ya siasa ikifanyika maeneo mbalimbali Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu amewataka viongozi wanaofanya mikutano hiyo kufanya kistaarabu.
Kingu ameyasema hayo Jumapili, Februari 5, 2023 wakati aliposhiriki kwenye mkutano wa kuadhimisha miaka 46 ya CCM mkoani Singida
uauliofanyikka kwenye wilaya ya Ikungi Jimbo la Singida Mashariki. -
Mbunge alia maduka ya kubadilisha fedha za kigeni
Mbunge wa Moshi Priscus Tarimo ameitaka Serikali kutoa wingu katika biashara ya maduka ya kubadilishia fedha za kigeni kwa kueleza sababu ni kwanini hawataki kutoa leseni kwa wafanyabiashara ingawa wamekidhi vigezo vipya.
Tarimo alikuwa akichangia leo Jumatatu Februari 6,2023 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Bajeti kwa Februari mwaka 2022 hadi Januari mwaka 2023. -
Luhaga Mpina amvaa tena Mwigulu Bungeni; Simbachawene aingilia kati amtega kwenye Vifungu
Vita ya maneno kati ya mbunge wa Kisesa na Waziri wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba bado ni mbichi ambapo leo Jumatatu Februari 6,2023 Mpina amemchokonoa tena Dk Mwigulu sasa akitaka akiomba bunge lipitishe Azimio la kuitaka Serikali kupeleka bungeni taarifa ya matumizi ya fedha zilizokopwa nje ya bajeti lakini akipendekeza Waziri wa Fedha awajibike.
Akochangia leo katika taarifa ya Kamati ya Bajeti, mbunge huyo amesema Kuna kusuasua katika usimamizi wa matumizi ya fedha ndiyo maana kumekuwa na malimbikizo ya deni la Taifa ambalo litapelekea riba kubwa kwa siku za usoni na hivyo kuongeza mfumuko wa bei. -
Sita wa familia moja ajali ya Korogwe wazikwa
Mamia ya wananchi katika Kitongoji cha Kirungu Mokala, Kata ya Kelamfua Mokala wilayani Rombo wamejitokeza kwenye mazishi ya marehemu Athanas Mrema (59) ambaye amezikwa yeye na mwanaye mmoja na mjukuu katika eneo moja.
Maziko hayo yamefanyika leo Februari 6, 2023 katika kitongoji cha Kirungu Mokala walipozikwa Athanas Mrema, Agustina Mrema, Tonny Mrema, Kennedy Mrema, Godfrey Mrema huku Nestory Kiwango amezikwa kijiji Cha Shimbi.
Ajali hiyo iliyoua watu 14 wa familia moja kati ya 20 ilitokea Februari 4, 2023 katika eneo la Magira Gereza, Kata ya Magira Gereza, wilayani Korogwe, Barabara ya Segera - Buiko mkoani Tanga.
Maoni Mapya